Featured

Loading...


Sakata la Z'bar Lakwamisha Vyama Vya Siasa Kumuaga Rais Kikwete


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imeahirisha kwa mara ya pili  hafla ya vyama vya siasa kumuaga Rais Jakaya Kikwete baada ya  kumaliza miaka 10 ya uongozi wake kwa mujibu wa katiba. 
 
Hafla hiyo inayoratibiwa na Baraza la Vyama vya Siasa ilipangwa  kufanyika jana baada ya Oktoba 2, mwaka huu kuahirishwa ili kutoa  fursa kwa Rais Kikwete kushughulikia mvutano wa uchaguzi wa Zanzibar  ulioibuka kufuatia Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kufuta matokeo  yote ya uchaguzi huo. 
 
Vyama vilivyoalikwa kushiriki hafla hiyo ya kumuaga Rais Kikwete ni  Chama Cha Mapinduzi (CCM), vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya  Wananchi ( Ukawa) vya Chadema, NCCR-Mageuzi, Cuf), NLD na vyama  vingine vya upinzani.
 
Akitangaza kuahirishwa kwa hafla hiyo  kwa mara ya pili, jijini Dar  es Salaam jana, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi,  alisema kikao hicho kimeahirishwa tena kutokana na Rais kubanwa  na  majukumu mengine ya kitaifa ikiwamo suala la Zanzibar.
 
 “Tumeamua kuahirisha  hadi siku tutakayotangaza tena kutokana na  Rais kukabiliwa na majukumu mengine na suala la Zanzibar bado  linashughulikiwa,” alisema.
 
Alisema akiwa msajili wa vyama vya siasa  amefurahishwa na hatua ya  Rais Kikwete  kulishughulikia suala la Zanzibar  kwa vitendo ili   kuhakikisha amani inaendelea kudumishwa  nchini.
~Mpekuzi blog

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright 2025 JICHO LETU | Designed By Code Nirvana
Back To Top